Swali: Kuna fadhilah maalum zilizothibiti kufanya ´Umrah katika miezi ya hajj zinazotofautiana na miezi mingine?
Jibu: Wakati mzuri zaidi wa kufanya ´Umrah ni ndani ya mwezi wa Ramadhaan. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”´Umrah ndani ya Ramadhaan ni sawa na hajj.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Imekuja katika upokezi wa al-Bukhaariy:
”´Umrah ndani ya Ramadhaan ni sawa na kuhiji nami.”
Bi maana pamoja na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Kisha baada ya hapo kuhiji katika Dhul-Qa´dah. Kwa sababu ´Umrah zake zote (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)zilifanyika katika Dhul-Qa´dah. Amesema (Subhaanah):
لَّقَدْ كَانَ لَكُمْ فِي رَسُولِ اللَّـهِ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ
“Hakika mna kigezo chema kwa Mtume wa Allaah.”[1]
[1] 33:21
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (15/324)
- Imechapishwa: 01/04/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)