Swali: Je, mfungaji akate swawm pale tu atakaposikia adhaana au asubiri mpaka imalizike?
Jibu: Kukiadhiniwa basi itafaa kwake kufungua. Isipokuwa akijua kuwa muadhini amekosea. Akiwa jangwani, akasikia adhaana lakini bado anaona jua, basi asifungue mpaka jua lizame. Lakini akiwa mjini pale muadhini anapoadhini umefika wakati wa kukata swawm. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Watu hawatoacha kuwa katika kheri muda wa kuwa wanaharakisha kukata swawm.”
Imekuja katika Hadiyth:
“Waja wanaopendeza zaidi kwangu ni wale waharakishao kukata swawm.”
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/audios/794/فتاوى-رمضانية
- Imechapishwa: 01/04/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)