2 – Si sahihi kufunga swawm ya faradhi isipokuwa kwa kulaza nia usiku. Imethibiti kutoka kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba amesema:
“Ambaye hakuazimia swawm kabla ya Fajr, basi hana swawm.”[1]
Imekuja katika tamko jingine:
“Ambaye hakulaza swawm kabla ya Fajr, basi hana swawm.”[2]
Imekuja katika tamko jingine:
“Ambaye hakulaza swawm sehemu ya usiku, basi hana swawm.”[3]
Imethibiti vilevile kwa al-Bukhaariy na Muslim ambao wamepokea kupitia kwa ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye ameeleza kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika hapana vyenginevyo matendo yanategemea nia na kila mmoja atalipwa vile alivyonuia.”[4]
[1] Abu Daawuud (2454).
[2] an-Nasaa´iy (2331).
[3] an-Nasaa´iy (2334).
[4] al-Bukhaariy (01) na Muslim (1907).
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Duruus fiy Ramadhwaan, uk. 14
- Imechapishwa: 11/04/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)