328 – ´Abdullaah bin ´Amr (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ameeleza kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
ستُّ مجالسَ؛ المؤمن ضامنٌ على الله تعالى ما كان في شيء منها: في مسجدِ جماعةٍ، وعند مريضٍ، أو في جنازةٍ، أو في بيتِهِ ، أو عندَ إمامٍ مُقْسِطٍ يُعَزِّرُهُ ويُوَقِّرُهُ، أو في مَشهدِ جهادٍ
“Allaah (Ta´ala) anamdhamini muumini muda wa kuwa anakuwa katika moja ya vikao vita: katika msikiti wa mkusanyiko, kwa mgonjwa, katika mazishi, katika nyumba yake[1], kwa kiongozi mwadilifu anayemtukuza na kumuheshimu au katika uwanja wa jihaad.”[2]
Ameipokea at-Twabaraaniy katika “al-Mu´jam al-Kabiyr” na al-Bazzaar kwa cheni ya wapokezi isiyokuwa nzuri hivo. Hata hivyo imepokelewa kupitia kwa Mu´aadh na wengineo kwa cheni ya wapokezi Swahiyh.
[1] Bi maana anakaa nyumbani kwake kwa kuepuka kushiriki shari. Kama ilivyo katika Hadiyth ya Mu´aadh aliyoashiria mtunzi wa kitabu. Inasema:
أو قعد في بيته؛ فَسَلم، وسَلِمَ الناس منه
“… au akakaa nyumbani kwake akasalimika yeye na watu wakasalimika naye.”
[2] Nzuri kupitia zingine.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/251)
- Imechapishwa: 05/12/2023
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket