Pili ni kwamba unamtetea al-Maghraawiy ambaye ni Takfiyr na anakufurisha kwa madhambi. Hivo ndivo yanadhihirisha maneno yake. Anaita madhambi yanayofanywa na waislamu kuwa:
“… ni kama uabudiaji ndama kama ndani ya wana wa israaiyl. Utiifu katika kumuasi Allaah ni uabudiaji sanamu.”[1]
Ina maana kwamba yule mwenye kumtii mtu amemfanya kuwa sanamu. Unamtetea na kusema:
“Anapozungumzia uabudiaji ndama na uabudiaji sanamu anaingia kwa ndani. Anapozungumza kwa baadhi ya matamshi ambayo udhahiri wake ni kuwakufurisha watenda madhambi, lau ningelikuwa simjui vyema Shaykh al-Maghraawiy, basi ningesema kuwa anakufurisha kwa madhambi. Ningesema hivo laiti ingelikuwa simjui, lakini mimi namjua. Kwa ajili hiyo mimi nafasiri maneno yake ya kijumla kutokana na ile ´Aqiydah yake ya wazi ninayoitambua wakati ninapozungumza naye. Hii ndio kanuni ambayo mimi naitambua, ya kwamba maneno ya wanamme yaliyokuja kwa jumla yanafasiriwa kwa maneno yao yaliyopambanuliwa.”[2]
Umesema wakati ulipokuwa ukimtukuza na kumkweza al-Maghraawiy:
“Nitawezaje kuondoa mlima na kusimamisha wakulima wa nyanya?”[3]
Hivyo ndivyo unaafikiana na wazuhi pindi unapowasifu, unawatapa na kukubaliana nao sambamba na kwamba unawajengea chuki Salafiyyuun na kuwatukana.
[1] Kaseti ”Mawaaqifu Ibraahiym” (3).
[2] Kaseti ”Munaaqashatu Ma’rib”.
[3] Kaseti ”Haqiyqat-ud-Da´wah” (2).
- Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Tanbiyh al-Wafiy ´alaa Mukhaalafaat Abiyl-Hasan al-Ma’ribiy, uk. 290-291
- Imechapishwa: 01/12/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)