341 – Umm Salamah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
خير مساجد النساءِ قَعْرُ بيتِهِن
“Bora ya misikiti ya wanawake ni ile sehemu ya ndani kabisa katika majumba yao.”[1]
Ameipokea Ahmad na at-Twabaraaniy katika ”al-Mu´jam al-Kabiyr”. Kwenye cheni yake ya wapokezi yuko Ibn Lahiy´ah. Ibn Khuzaymah pia ameipokea katika ”as-Swahiyh” yake na al-Haakim kupitia kwa Darraaj Abus-Samh, kutoka kwa as-Saa-ib, mtumwa wa Umm Salamah aliyemwacha huru. Ibn Khuzaymah amesema:
“Sijui juu ya kusifiwa wala kujeruhiwa kwa as-Saa-ib, mtumwa wa Umm Salamah aliyemwacha huru.”
al-Haakim amesema:
“Cheni yake ya wapokezi ni Swahiyh.”
[1] Nzuri kupitia zingine.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/259)
- Imechapishwa: 17/12/2023
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)