Swali: Inafaa kwa mwanafunzi kuwaasi wazazi wake katika kutafuta elimu?

Jibu: Linahitaji upambanuzi. Ikiwa anafuta elimu katika yale mambo yanayomlazimu:

“Hakuna utiifu kwa kiumbe katika kumuasi Muumba.”

Lakini ikiwa ni katika kujizidishia elimu na kubobea katika elimu, akusanye kati ya mambo mawili: asiwaasi wazazi wawili katika kule kumuhitaji na atafute elimu kwa kiasi cha uwezo wake. Akusanye kati ya mambo mawili. Lakini katika kujifunza elimu yake na katika yale ambayo hapewi udhuru kutoyajua, inamlazimu. Katika hali hiyo haifai kwake kumtii yeyote. Hakika si vyengine utiifu unakuwa katika mema tu.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23512/هل-تجوز-معصية-الوالدين-في-طلب-العلم
  • Imechapishwa: 03/02/2024