Swali: Je, Aakhirah watu watajuana kama jinsi walivyokuwa wakijuana duniani?
Jibu: Bila ya shaka Aakhirah watajuana kati yao:
وَيَوْمَ يَحْشُرُهُمْ كَأَن لَّمْ يَلْبَثُوا إِلَّا سَاعَةً مِّنَ النَّهَارِ
“Na [wakumbushe] Siku atakayowakusanya [wataona] kama kwamba hawakuishi [duniani] isipokuwa saa moja ya mchana.” (10:45)
Watajuana kati yao. Watajuana wao kwa wao. Baba atamjua mtoto wake na mtu atamjua kaka yake. Lakini hakuna yeyote ataweza kumsaidia mwenzie:
يَوْمَ يَفِرُّ الْمَرْءُ مِنْ أَخِيهِ
“Siku mtu atakapomkimbia ndugu yake.” (80:34)
يُبَصَّرُونَهُمْ ۚ يَوَدُّ الْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِي مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذٍ بِبَنِيهِ
“Watafanywa waonane, [lakini] mhalifu atatamani ajikomboe na adhabu siku hiyo kwa [kuwatoa] watoto wake.” (70:11)
Watafanywa waonane kati yao. Haina shaka yoyote kuwa watajuana. Lakini hata hivyo hakuna yeyote ataweza kumsaidia mwenzie katika kisimamo hicho na siku hiyo. Kila mmoja atakuwa ni mwenye kushughulishwa na matendo yake.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (49) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1431-6-3.mp3
- Imechapishwa: 21/08/2020
Swali: Je, Aakhirah watu watajuana kama jinsi walivyokuwa wakijuana duniani?
Jibu: Bila ya shaka Aakhirah watajuana kati yao:
وَيَوْمَ يَحْشُرُهُمْ كَأَن لَّمْ يَلْبَثُوا إِلَّا سَاعَةً مِّنَ النَّهَارِ
“Na [wakumbushe] Siku atakayowakusanya [wataona] kama kwamba hawakuishi [duniani] isipokuwa saa moja ya mchana.” (10:45)
Watajuana kati yao. Watajuana wao kwa wao. Baba atamjua mtoto wake na mtu atamjua kaka yake. Lakini hakuna yeyote ataweza kumsaidia mwenzie:
يَوْمَ يَفِرُّ الْمَرْءُ مِنْ أَخِيهِ
“Siku mtu atakapomkimbia ndugu yake.” (80:34)
يُبَصَّرُونَهُمْ ۚ يَوَدُّ الْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِي مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذٍ بِبَنِيهِ
“Watafanywa waonane, [lakini] mhalifu atatamani ajikomboe na adhabu siku hiyo kwa [kuwatoa] watoto wake.” (70:11)
Watafanywa waonane kati yao. Haina shaka yoyote kuwa watajuana. Lakini hata hivyo hakuna yeyote ataweza kumsaidia mwenzie katika kisimamo hicho na siku hiyo. Kila mmoja atakuwa ni mwenye kushughulishwa na matendo yake.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (49) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1431-6-3.mp3
Imechapishwa: 21/08/2020
https://firqatunnajia.com/watu-siku-ya-qiyaamah-watajuana/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)