Swali: Mwenye kupinga kuwa Allaah Ataonekana Aakhirah anakufuru au anaambiwa kuwa ni mtu wa Bid´ah?

Jibu: Akizijua dalili na akapinga kuonekana ilihali anajua dalili, anakufuru kwa kuwa yamepokelewa kwa mapokezi mengi (Mutawaatir). Ama ikiwa ni mfuata kichwa mchunga au ni mjinga, huyu anakuwa mpotevu. Hakufurishwi isipokuwa mpaka baada ya kubainishiwa dalili. Akiendelea kupinga baada ya kubainishiwa, anakufuru.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (49) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1431-6-3.mp3
  • Imechapishwa: 21/08/2020