Swali: Waswaliji husimama pale tu wanapomuona imamu ameingia mlango wa msikiti.
Jibu: Ikiwa desturi ya imamu ni kwamba anapoingia ndio hukimiwa swalah, basi wasisimame mpaka kukimiwe swalah ingawa wamemuona ameingia. Kwa sababu Bilaal alikuwa anapomuona (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ameingia hukimu swalah. Lakini wakati mwingine anaweza kukimu kabla ya imamu kuingia kwa mujibu wa miadi iliopo baina yake na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)… Kwa hivyo wasisimame mpaka wamemuona imamu ameingia.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23710/حكم-قيام-المامومين-عند-دخول-الامام-المسجد
- Imechapishwa: 07/04/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)