Mtu mwenye busara ni yule mwenye kukubali wasia wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na ambaye anapupia juu ya yale yenye kumnufaisha. Ni wingi uliyoje wa wale wenye kutumia wakati wao katika mambo yasiyokuwa na faida! Bali wanatumia wakati wao katika mambo yaliyo na madhara juu ya nafsi zao na dini yao. Kwa ajili hii tunawaambia watu hawa kuwa hawakutendea kazi wasia wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Wanafanya hivo ima kwa kutokujua au kwa kupuuza. Lakini hata hivyo muumini mwenye busara ni yule anayekubali wasia kama huu na anapupia juu ya yale mambo yenye kumnufaisha katika dini na dunia yake.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Riyaadh-is-Swaalihiyn (02/78-79)
- Imechapishwa: 01/11/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)