Swali: Ni ipi hukumu ya msemo:
”Wapenzi kwa ajili ya Mtume wa Allaah?”
Jibu: Msemo huu, ijapo inanidhihirikia kuwa mwenye nayo anakusudia maana sahihi, anachokusudia ni kwamba tumekusanyika sote katika kumpenda kwetu Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Lakini hata hivyo ibara hii ni kinyume na yale yaliyopokelewa katika Sunnah. Hadiyth inasema:
”Anayependa kwa ajili ya Allaah na akachukia kwa ajili ya Allaah… ”
Kinachompasa ni yeye kusema ”wapenzi kwa ajili ya Allaah (´Azza wa Jall).” Isitoshe msemo huu ni kuacha yale waliyokuwa wanayasema Salaf. Pengine yakapelekea katika kuchupa mpaka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kughafilika kutokana na Allaah. Kinachotambulika kwa wanazuoni wetu na kwa watu wema ni yeye kusema ”wapenzi kwa ajili ya Allaah”.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Manaahiy al-Lafdhwiyyah, uk. 04-05
- Imechapishwa: 01/07/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)