Swali: Je, wanapata dhambi wale ambao wanazungumza na kucheka wakati ambapo watu wanaswali Tarawiyh katika msikiti Mtakatifu?
Jibu: Hapana, hawapati dhambi. Swalah ya Tarawiyh ni yenye kupendeza na sio faradhi. Lakini muhimu wasiwashawishi waswaliji. Wajibu kwao ni kutoshawishi. Hata hivyo hapana neno ikiwa pembezoni mwao hakuna mtu yeyote anayeshawishi.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22791/حكم-من-يتكلمون-بالمسجد-اثناء-صلاة-التراويح
- Imechapishwa: 24/08/2023