“Ukienda kwa familia yako basi wewe umeachika”

Swali: Ni ipi hukumu ambaye amemwambia mke wake “ukienda kwa familia yako basi wewe umetalikika” kisha wakati wa kutokuweko kwa mume mke akaenda kwa familia yake?

Jibu: Mume akimwambia mke wake “ukienda kwa familia yako basi wewe umetalikika”, ataulizwa makusudio yake; amekusudia kumkataza peke yake au amekusudia akienda kweli talaka imepita? Kama amekusudia kumkataza kwenda na neno talaka amekusudia kumtisha na sio kuikusudia, lakini ni kwa lengo la kumdhibiti na hakukusudia talaka kabisa, basi tunamwambia atoe kafara ya kiapo na hakuna kingine kilichotokea. Akisema kuwa alichokusudia ni kupita kwa talaka endapo mwanamke huyo ataenda, basi talaka itakuwa imepita.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah Aalish-Shaykh
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://www.mufti.af.org.sa/ar/content/حكم-قول-من-قال-لزوجته-إذا-ذهبتي-إلى-أهلك-فأنت-طالق
  • Imechapishwa: 11/06/2022