Wanawaita Salafiyyuun “Khawaarij” pamoja na kuwa Salafiyyuun usiku na mchana wanapiga vita madhehebu ya Khawaarij. Lakini pamoja na hivyo bado tu wanasema Salafiyyuun ndio Khawaarij. Wanasema wao ndio “Murji-ah” pamoja na kuwa wanapiga vita Irjaa´. Wanasema “Ni makafiri” pamoja na kuwa wanawapiga vita makafiri. Vipi mtu anaweza kunyamazia hili?

Uislamu unawakilishwa kwa Manhaj ya Salaf na sio Manhaj ya al-Ikhwaan, at-Tabliygh, Qutbiyyuun, Manhaj ya Abul-Hasan na kundi lake kwa sababu wao wenyewe wako pamoja na Khawaarij na ni katika wachezaji wakubwa na wenye kuwatetea Ahl-ul-Bid´ah na wamefikia mpaka kutetea kanuni za batili.

Watu wote hawa wana majanga yanayowaweka mbali kabisa na Manhaj ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah. Wanatatiza na wanajinasibisha katika Manhaj ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah kwa uongo.

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: adh-Dhariy´ah ilaa Bayaan Maqaasid Kitaab-ish-Sharï´ah (1/
  • Imechapishwa: 19/05/2015