Swali: Je, inafaa kutibu uchawi kwa kutumia uchawi?
Jibu: Hapana. [´Imraan bin Huswayn (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:]
”Si katika sisi yule atakayeamini mikosi au akaomba kubashiriwa mikosi, akafanya uchawi au akafanyiwa uchawi, akafanya ukuhani au akafanyiwa ukuhani.”[1]
Kutibu uchawi kwa uchawi ni haramu. Hakuna anayefumbua uchawi isipokuwa mchawi. Haijuzu kufanya hivo. Uchawi unatibiwa kwa njia zinazoruhusiwa, kama vile dhikr, Qur-aan na du´aa zinazotambuliwa na wale wenye taaluma hiyo.
[1] al-Bazzaar (3578), ad-Duulaabiy (2083) na at-Twabaraaniy katika “al-Mu´jam al-Awsatw” (355).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (42)
- Imechapishwa: 15/12/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)