Endapo utaulizwa nini maana ya Twaa Haa? Utasema kuwa haina maana katika lugha ya kiarabu. Ni herufi za mkato zinazojulisha kwamba waarabu wameshindwa kuleta mfano wa Qur-aan.
Kuhusu waliosema kuwa Twaa Haa ni miongoni mwa majina ya Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hana dalili. Ametamka kitu asichokijua. Haikupokelewa kwamba miongoni mwa majina ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni Twaa Haa. Endapo atasema: ”Allaah si ndiye ambaye amesema:
طه مَا أَنزَلْنَا عَلَيْكَ الْقُرْآنَ لِتَشْقَىٰ
“Twaa Haa. Hatukukuteremshia Qur-aan ili upate mashaka.”?[1]
Nasi tutamuuliza kama Yaa Siyn pia ni jina lake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa sababu Allaah amesema:
يس وَالْقُرْآنِ الْحَكِيمِ
”Yaa Siyn. Naapa kwa Qur-aan yenye hekima.”?[2]
Tutamuuliza pia kama Nuun ni jina lake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa sababu Allaah amesema:
ن ۚ وَالْقَلَمِ وَمَا يَسْطُرُونَ
”Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo.”?[3]
Tutamuuliza pia kama Aliyf Laam Miym Swaad ni jina lake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa sababu Allaah amesema:
المص كِتَابٌ أُنزِلَ إِلَيْكَ
”Alif Laam Miym Swaad. Hiki Kitabu kimeteremshwa kwako.”?[4]
Hakuna yeyote awezaye kusema hivo.
Napenda kuwaambia ndugu zangu kwamba majina yote ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yametokana na maana kuu. Muhammad na Ahmad yanatokana na kusifiwa, al-Haashir mwenye kuwakusanya watu, al-Aaqib ambaye hakuna baada yake Nabii na kadhalika. Majina yote ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yametokana na maana kuu na tukufu. Vivyo hivyo majina ya Qur-aan. Hali kadhalika majina ya Mola (´Azza wa Jall). Yote yanatokana na maana tukufu na kuu. Hutopata ndani yake jina lisilokuwa na maana yoyote.
[1] 20:01-02
[2] 36:01-02
[3] 68:01
[4] 07:01-02
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://www.youtube.com/watch?v=S-TedIc4EDI
- Imechapishwa: 12/12/2020
Endapo utaulizwa nini maana ya Twaa Haa? Utasema kuwa haina maana katika lugha ya kiarabu. Ni herufi za mkato zinazojulisha kwamba waarabu wameshindwa kuleta mfano wa Qur-aan.
Kuhusu waliosema kuwa Twaa Haa ni miongoni mwa majina ya Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hana dalili. Ametamka kitu asichokijua. Haikupokelewa kwamba miongoni mwa majina ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni Twaa Haa. Endapo atasema: ”Allaah si ndiye ambaye amesema:
طه مَا أَنزَلْنَا عَلَيْكَ الْقُرْآنَ لِتَشْقَىٰ
“Twaa Haa. Hatukukuteremshia Qur-aan ili upate mashaka.”?[1]
Nasi tutamuuliza kama Yaa Siyn pia ni jina lake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa sababu Allaah amesema:
يس وَالْقُرْآنِ الْحَكِيمِ
”Yaa Siyn. Naapa kwa Qur-aan yenye hekima.”?[2]
Tutamuuliza pia kama Nuun ni jina lake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa sababu Allaah amesema:
ن ۚ وَالْقَلَمِ وَمَا يَسْطُرُونَ
”Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo.”?[3]
Tutamuuliza pia kama Aliyf Laam Miym Swaad ni jina lake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa sababu Allaah amesema:
المص كِتَابٌ أُنزِلَ إِلَيْكَ
”Alif Laam Miym Swaad. Hiki Kitabu kimeteremshwa kwako.”?[4]
Hakuna yeyote awezaye kusema hivo.
Napenda kuwaambia ndugu zangu kwamba majina yote ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yametokana na maana kuu. Muhammad na Ahmad yanatokana na kusifiwa, al-Haashir mwenye kuwakusanya watu, al-Aaqib ambaye hakuna baada yake Nabii na kadhalika. Majina yote ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yametokana na maana kuu na tukufu. Vivyo hivyo majina ya Qur-aan. Hali kadhalika majina ya Mola (´Azza wa Jall). Yote yanatokana na maana tukufu na kuu. Hutopata ndani yake jina lisilokuwa na maana yoyote.
[1] 20:01-02
[2] 36:01-02
[3] 68:01
[4] 07:01-02
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://www.youtube.com/watch?v=S-TedIc4EDI
Imechapishwa: 12/12/2020
https://firqatunnajia.com/twaaha-na-yaasiyn-sio-majina-ya-mtume/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)