Kuhusiana na kwamba wanafanana na jamii kwa mtu ambaye yuko anazama na wanafunzi na wanachuoni kwa mtu ambaye anamkataza, wanachotaka ni sisi tunyoe ndevu zetu ili tuwe walaini na wepesi. Wanachotaka ni sisi tununue TV na tuiweke nyumbani ili wanawake wetu waweze kuangalia TV na sisi tuangalie wasichana warembo. Wanataka pia tuvae suruwali, kujiunga katika jeshi hata kama itakuwa na maana ya kutumbukia katika maasi na kuikanyaga Sunnah. Watu wapuuzi! Je, njaa inatokana na umasikini kwa ajili ya dini au ni madhambi? Allaah (Tabaaraka wa Ta´ala) Amesema:

وَضَرَبَ اللَّـهُ مَثَلًا قَرْيَةً كَانَتْ آمِنَةً مُّطْمَئِنَّةً يَأْتِيهَا رِزْقُهَا رَغَدًا مِّن كُلِّ مَكَانٍ فَكَفَرَتْ بِأَنْعُمِ اللَّـهِ فَأَذَاقَهَا اللَّـهُ لِبَاسَ الْجُوعِ وَالْخَوْفِ بِمَا كَانُوا يَصْنَعُونَ

”Allaah amepiga mfano wa mji uliokuwa katika amani na utulivu, inaifikia riziki yake maridhawa kutoka kila mahali; ukakufuru neema za Allaah basi Allaah akauonjesha funiko la njaa na khofu kwa yale waliyokuwa wakitenda.” (16:112)

al-Ikhwaan al-Muslimuun wanapiga ndege mbili kwa jiwe moja; ujinga na upotevu. Siku moja alikuja kijana mmoja wa al-Ikhwaan al-Muslimuun ili kutupeleleza. Nikamwambia:

”Leta karatasi ili niweze kuandika kuwa Da´wah ya al-Ikhwaan al-Muslimuun imejengwa juu ya ujinga na upotevu, hivyo utaacha kujichosha bure.”

  • Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fadhwaaih wa Naswaaih, uk. 22-23
  • Imechapishwa: 26/08/2020