Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah wameyakusanya maandiko na wakagawa matakwa katika vigawanyo viwili (matakwa ya Kishari´ah na ya kilimwengu). Hawakufanya hivo kujitolea kwao wenyewe, bali wameyatoa kwenye maandiko.
Matakwa ya kilimwengu ni yale yenye kutajwa na waislamu kwenye msemo wao: “Anayoyataka Allaah huwa, Asiyoyataka hayawi”.
Kuhusu matakwa ya kidini na Kishari´ah, ni yale yenye kutajwa na watu: “Huyu anafanya mambo Asiyoyataka Allaah” wakiwa na maana ya kwamba anafanya mambo Asiyoyapenda Allaah. Kwa ajili hii lau mtu atasema: “Nitafanya kitu kadhaa Allaah akitaka [in shaa Allaah]” kisha asikifanye, hana juu yake kitu. Haijalishi kitu hata kama hicho alichotaka kufanya ilikuwa ni kitu cha wajibu au cha Sunnah. Akisema: “Wallaahi nitaswali Dhuhaa Allaah akitaka” na kisha asiswali, hana juu yake kitu kwa kuwa amefungamanisha na matakwa [ya Allaah ambayo ni ya kilimwengu]. Lakini akisema: “Nitaswali Dhuhaa Allaah akipenda [in ahabba Allaah]” na kisha asiswali, juu yake ni lazima kutoa kafara ya yamini kwa kuwa Allaah anapenda aswali Dhuhaa.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajhiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Hidaayah ar-Rabbaaniyyah fiy Sharh al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah (01/57)
- Imechapishwa: 07/06/2020
Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah wameyakusanya maandiko na wakagawa matakwa katika vigawanyo viwili (matakwa ya Kishari´ah na ya kilimwengu). Hawakufanya hivo kujitolea kwao wenyewe, bali wameyatoa kwenye maandiko.
Matakwa ya kilimwengu ni yale yenye kutajwa na waislamu kwenye msemo wao: “Anayoyataka Allaah huwa, Asiyoyataka hayawi”.
Kuhusu matakwa ya kidini na Kishari´ah, ni yale yenye kutajwa na watu: “Huyu anafanya mambo Asiyoyataka Allaah” wakiwa na maana ya kwamba anafanya mambo Asiyoyapenda Allaah. Kwa ajili hii lau mtu atasema: “Nitafanya kitu kadhaa Allaah akitaka [in shaa Allaah]” kisha asikifanye, hana juu yake kitu. Haijalishi kitu hata kama hicho alichotaka kufanya ilikuwa ni kitu cha wajibu au cha Sunnah. Akisema: “Wallaahi nitaswali Dhuhaa Allaah akitaka” na kisha asiswali, hana juu yake kitu kwa kuwa amefungamanisha na matakwa [ya Allaah ambayo ni ya kilimwengu]. Lakini akisema: “Nitaswali Dhuhaa Allaah akipenda [in ahabba Allaah]” na kisha asiswali, juu yake ni lazima kutoa kafara ya yamini kwa kuwa Allaah anapenda aswali Dhuhaa.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajhiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Hidaayah ar-Rabbaaniyyah fiy Sharh al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah (01/57)
Imechapishwa: 07/06/2020
https://firqatunnajia.com/tofauti-ya-akitaka-allaah-na-akipenda-allaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)