Swali: Thawabu za swadaqah yenye kuendelea zinasimama kwa kusimama sababu yake kwa mfano yakakauka ndani ya kisima? Aidha elimu ambayo watu wananufaika nayo zinasimama thawabu zake kwa kusimama sababu yake?
Jibu: Midhali watu wananufaika nayo basi thawabu ni zenye kubakia. Ikikatika basi thawabu pia zinasimama.
Swali: Thawabu haziendelei?
Jibu: Zinasimama kwa kusimama thawabu zake.
Swali: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Anapofariki mwanadamu basi matendo yake yote hukatika isipokuwa vitu vitatu; swadaqah yenye kuendelea, elimu ambayo watu wananufaika kwayo au mtoto mwema anayemuombea du´aa.”
Je, swadaqah yenye kuendelea na elimu ambayo watu wananufaika kwayo vinalingana au hakuna tofauti kati ya hayo mawili?
Jibu: Allaah ndiye mjuzi zaidi. Muhimu anapata thawabu kwa Allaah.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22974/هل-ينقطع-اجر-الصدقة-والعلم-بانقطاع-السبب
- Imechapishwa: 23/09/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)