Swali: Ambaye ana upeo wa kufanya tarjama ya maana ya Qur-aan Tukufu. Pale ambapo Aayah moja itakuwa na maana zaidi ya moja na wafasiri wa Qur-aan wakatofautiana katika kuifasiri, mwenye kufanya tarjama atachagua maoni yepi katika kufasiri Aayah hiyo?
Jibu: Enyi ndugu! Tarjama haina maana ya mtu aende kufasiri Qur-aan. Mwenye kufanya tarjama anachotakiwa ni kuleta kitabu miongoni mwa vitabu vya Tafsiyr kinachoaminiwa – iwe ni kitabu kinachoaminiwa – ndio atarjumu [kupitia kitabu hicho]. Asitarjumu kwa mujibu wake. Haifai kwake kutarjumu kwa mujibu wake. Anachotakiwa ni kutarjumu kwa kupitia Tafsiyr miongoni mwa Tafsiyr zenye kuaminika. Kwa ajili hii ndio maana inaitwa “Tarjama ya maana ya Qur-aan Tukufu” na sio tarjama ya Qur-aan. Hakuna anayejua tarjama ya maana ya Qur-aan Tukufu isipokuwa wafasiri wahakiki. Ama mtarjumu yeye huwa ni mwenye kunukuu tu kutoka kwenye lugha na kwenda lugha nyingie. Hivyo basi, asitarjumu na kufasiri kwa mujibu wake.
Kumepatikana makosa mengi kutoka kwa watu hawa katika kutarjumu kwao Qur-aan kwa sababu wameegemea ufahamu wao. Kumepatikana makosa mengi katika tarjumu kwa sababu hii.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (14) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1427-10-15.mp3
- Imechapishwa: 19/08/2020
Swali: Ambaye ana upeo wa kufanya tarjama ya maana ya Qur-aan Tukufu. Pale ambapo Aayah moja itakuwa na maana zaidi ya moja na wafasiri wa Qur-aan wakatofautiana katika kuifasiri, mwenye kufanya tarjama atachagua maoni yepi katika kufasiri Aayah hiyo?
Jibu: Enyi ndugu! Tarjama haina maana ya mtu aende kufasiri Qur-aan. Mwenye kufanya tarjama anachotakiwa ni kuleta kitabu miongoni mwa vitabu vya Tafsiyr kinachoaminiwa – iwe ni kitabu kinachoaminiwa – ndio atarjumu [kupitia kitabu hicho]. Asitarjumu kwa mujibu wake. Haifai kwake kutarjumu kwa mujibu wake. Anachotakiwa ni kutarjumu kwa kupitia Tafsiyr miongoni mwa Tafsiyr zenye kuaminika. Kwa ajili hii ndio maana inaitwa “Tarjama ya maana ya Qur-aan Tukufu” na sio tarjama ya Qur-aan. Hakuna anayejua tarjama ya maana ya Qur-aan Tukufu isipokuwa wafasiri wahakiki. Ama mtarjumu yeye huwa ni mwenye kunukuu tu kutoka kwenye lugha na kwenda lugha nyingie. Hivyo basi, asitarjumu na kufasiri kwa mujibu wake.
Kumepatikana makosa mengi kutoka kwa watu hawa katika kutarjumu kwao Qur-aan kwa sababu wameegemea ufahamu wao. Kumepatikana makosa mengi katika tarjumu kwa sababu hii.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (14) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1427-10-15.mp3
Imechapishwa: 19/08/2020
https://firqatunnajia.com/tarjama-za-qur-aan-nyingi-leo-zina-makosa-tele/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)