Talaka wakati wa hasira kali

Swali: Ni ipi hukumu ya talaka ya hasira kali ambayo mwenye kutoa huwa na tabia ya kutomiliki nafsi yake wakati huo?

Jibu: Tayari limezungumzwa jambo hili. Wanazuoni wamekhitalifiana kuhusu hilo. Maoni yenye nguvu zaidi ni kwamba talaka haikupita. Ikiwa hasira imezidi sana, ikamfunga akili na nia yake, akashindwa kujimiliki kabisa na kukawa na dalili zinazoonyesha hali hiyo. Kwa sababu hali halisi huwa ina sababu zake. Ikiwa zipo sababu zinazoonyesha kweli hasira ilizidi na akili ikafungika, basi talaka haipiti. Ikiwa hakuna dalili hizo, basi hukumu hutofautiana.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1307/حكم-الطلاق-حال-الغضب-المغلق
  • Imechapishwa: 20/06/2026