Swali: Je, inafaa kuswali Rak´ah mbili za mamkuzi ya msikiti na sisi tunaenda kuswali ´iyd msikitini au haifai kuswali Rak´ah mbili katika swalah ya ´iyd?
Jibu: Kiwanja cha kuswalia ´iyd hakina mamkuzi ya msikiti. Hakina hukumu moja kama misikiti. Hakina mamkuzi ya msikiti. Bali mtu anatakiwa kuketi chini. Isitoshe wakati huo mtu amekatazwa kuswali. Kiwanja cha kuswalia ´iyd sio msikiti. Lakini ikiwa swalah ya ´iyd inaswaliwa katika msikiti wa kawaida na uliozoeleka, wakiswali ´iyd kwenye misikiti basi kumesuniwa kuswali swalah ya mamkuzi ya msikiti ijapo ni katika wakati ambapo mtu amekatazwa kuswali kwa mujibu wa maoni sahihi. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Anapoingia mmoja wenu msikiti basi asiketi chini mpaka kwanza aswali Rak´ah mbili.”
Wakati siku moja (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipomwona bwana mmoja ameketi chini alimwambia:
“Simama na uswali Rak´ah mbili.”
Kuhusu kiwanja cha kuswalia ´iyd kinachokuwa jangwani hakina hukumu moja kama msikiti. Kwa hivyo mtu akija na jua halijachomoza, basi ataketi chini. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa haswali swalah ya ´iyd si kabla wala baada yake.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/16566/مصلى-العيد-ليس-له-تحية
- Imechapishwa: 29/04/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket