Swali: Je, inafaa kuwatukana Ahl-ul-Bid´ah na kuwaeleza kwa njia inayopelekea matusi wakati wa kutahadharisha nao?
Jibu: Hakuna haja ya kulaani. Hili halitatui tatizo. Hata hivo yanatakiwa kubainishwa makosa walionayo. Ubainifu na matahadharisho juu ya Bid´ah zao inatakiwa iwe kwa njia ya kielimu ili watu wasitumbukie katika Bid´ah zao na hivyo wakaangamia. Asiwatukane na wala asiwashutumu. Bali abainishe makosa yao na kwenda kwao kinyume.
Bid´ah zinatofautiana. Kuna Bid´ah kubwa ambazo mwenye nazo anatukanywa na kutahadharishwa. Bid´ah nyenginezo hazifikii kiwango hicho. Hata hivyo kosa la mzushi huyo linatakiwa kubainishwa. Na ikiwa ni miongoni mwa wanaozilingania, basi anapaswa kutahadharishwa.
- Muhusika: ´Allaamah Zayd bin Muhammad al-Madkhaliy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://www.youtube.com/watch?app=desktop&v=4i3YojbP2rk
- Imechapishwa: 17/02/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)