Swali: Kuna profesa ambaye kasema kuwa swalah ya Tarawiyh haiwi kwa mkusanyiko.
Jibu: Sunnah katika swalah ya Tarawiyh iswaliwe msikitini mkusanyiko. Hivo ndivo alivofanya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika baadhi ya nyusiku mwezi wa Ramadhaan. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwaswalisha Maswahabah nyusiku tatu na usiku wa nne (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakutoka na akasema:
“Nimechelea isije kufaradhishwa kwenu.”
Wakati wa uongozi wa ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) aliwaona watu wanaswali kila mmoja akiswali kivyake ambapo akasema:
“Lau ningewakusanya nyuma ya imamu mmoja.”
Akamwamrisha Ubayy awaswalishe watu. Sababu iliyomzuia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuendelea na swalah ya Tarawiyh imekwishaondoka. Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) wameafikiana juu ya kile alichoona ´Umar na wakaona kuwa kitendo hicho ni kuhuisha Sunnah ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hakuna mwanachuoni yeyote wa Kiislamu, hapo zamani na hivi sasa, ambaye ameonelea kinyume na hivo.
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
´Abdullaah bin Ghudayyaan
Swaalih al-Fawzaan
´Abdul-´Aziyz Aalish-Shaykh
Bakr Abu Zayd
- Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (06/80) nr. (17882)
- Imechapishwa: 22/04/2022
Swali: Kuna profesa ambaye kasema kuwa swalah ya Tarawiyh haiwi kwa mkusanyiko.
Jibu: Sunnah katika swalah ya Tarawiyh iswaliwe msikitini mkusanyiko. Hivo ndivo alivofanya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika baadhi ya nyusiku mwezi wa Ramadhaan. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwaswalisha Maswahabah nyusiku tatu na usiku wa nne (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakutoka na akasema:
“Nimechelea isije kufaradhishwa kwenu.”
Wakati wa uongozi wa ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) aliwaona watu wanaswali kila mmoja akiswali kivyake ambapo akasema:
“Lau ningewakusanya nyuma ya imamu mmoja.”
Akamwamrisha Ubayy awaswalishe watu. Sababu iliyomzuia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuendelea na swalah ya Tarawiyh imekwishaondoka. Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) wameafikiana juu ya kile alichoona ´Umar na wakaona kuwa kitendo hicho ni kuhuisha Sunnah ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hakuna mwanachuoni yeyote wa Kiislamu, hapo zamani na hivi sasa, ambaye ameonelea kinyume na hivo.
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
´Abdullaah bin Ghudayyaan
Swaalih al-Fawzaan
´Abdul-´Aziyz Aalish-Shaykh
Bakr Abu Zayd
Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (06/80) nr. (17882)
Imechapishwa: 22/04/2022
https://firqatunnajia.com/swalah-ya-tarawiyh-ni-mkusanyiko/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)