Hatusomi Qur-aan kwa njia ya kuizingatia na kuwaidhika na yaliyomo ndani. Waislamu wengi wanasoma Qur-aan kwa ajili ya kutafuta baraza zake na kutaka thawabu tu. Linalotakikana ni sisi kusoma Qur-aan kwa mazingatio na kwa ajili ya kuwaidhika na yaliyomo ndani. Allaah (Ta´ala) amesema:
كِتَابٌ أَنزَلْنَاهُ إِلَيْكَ مُبَارَكٌ
“Kitabu Tumekiteremsha kwako chenye baraka… ”
Huu ni ujira.
لِّيَدَّبَّرُوا آيَاتِهِ
”… ili wapate kuzingatia kwa makini Aayah zake… ”
Haya ndio matunda.
وَلِيَتَذَكَّرَ أُوْلُوا الْأَلْبَابِ
”… na ili wapate kukumbuka wale wenye akili.”[1]
[1] 38:29
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Riyaadh-is-Swaalihiyn (02/142)
- Imechapishwa: 29/04/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket