Swali: Je, ni kweli kwamba umesifu kitabu ”as-Siraaj al-Wahhaaj fiy Swahiyh-il-Minhaaj” cha Abul-Hasan al-Miswriy?
Jibu: Minhaaj ipi? Mimi ndio mara ya kwanza nakisikia. Ni vipi nikisifu? Naapa kwa Allaah kwamba ndio mara ya kwanza nakisikia. Kitabu ninachokijua ni ”as-Siraaj al-Wahhaaj min Kashf Matwaalib Swahiyh Muslim bin al-Hajjaaj” cha Siwddiyq Hasan Khaaan. Kuhusu kitabu hichi mimi sikijui. Lakini leo ni rahisi kusema uwongo na uzushi. Tusithibtishe maneno yoyote juu yangu mimi wala mwingine yeyote mpaka mwenye nayo alete maandishi, saini au sauti iliyorekodiwa. Pamoja na kwamba sauti pia inaweza kugilizwa, lakini mtu anaweza kupuuzilia jambo hilo. Msiamini uvumi unaoenezwa. Mnaona uwongo leo ni mwingi na kugombanisha kati ya wanazuoni. Tahadharini na jambo hili.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Tatwhiyr-il-I´tiqaad (8) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/et–1432-04-03.mp3
- Imechapishwa: 12/11/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)