Sema wazi kwamba sauti yako ndio imeumbwa na si Qur-aan

Swali: Vipi kuhusu mwenye kusema kuwa kisomo chake na matamshi yake ya kisomo cha Qur-aan yameumbwa?

Jibu: Anatakiwa kusema wazi sauti yake anayosoma ndio imeumbwa. Lakini Qur-aan haikuumbwa. Akisema matamshi yake kunaleta sintofahamu. Mtu anaweza kufikiri kuwa anakusudia kile kinachotamkwa. Aseme wazi kwamba sauti yake ndio imeumbwa. Kuhusu Qur-aan ni maneno ya Allaah na hayakuumbwa.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Ta´liyqaat ´alaal-Fatwaa al-Hamawiyyah al-Kubraa, uk. 156
  • Imechapishwa: 16/02/2023