Swali: Ni ipi hukumu ya kuwatolea salamu Ahl-ul-Bid´ah, kukaa nao na kutembea nao?
Jibu: Ni wajibu kuwasusa Ahl-ul-Bid´ah. Ikiwa hawakutubu baada ya kuwanasihi haijuzu kukaa nao ili asije kumuathiri. Ni wajibu kuwasusa.
Lakini hata hivyo ni lazima tujue ni nini Bid´ah. Baadhi ya watu hawajui Bid´ah ni kitu gani. Kila mwenye kutofautiana naye au kutokubali maoni yake anamfanyia Tabdiy´. Sivyo hivyo. Bid´ah imebainishwa na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa salla) pale aliposema:
“Atakayezusha katika dini yetu hii yasiyokuwemo atarudishiwa mwenyewe.”
“Tahadharini na mambo ya kuzua. Hakika kila kitakachozushwa ni Bid´ah na kila Bid´ah ni upotevu.”
Bid´ah ni kile chenye kwenda kinyume na Sunnah.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Duruus-ul-Haram http://www.alfawzan.af.org.sa/node/13385
- Imechapishwa: 24/06/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)