Swali: Mtu ambaye shaytwaan amemshawishi na akamwende mwanamke ambaye ni ajinabi na mapenzi bila ya jimaa kitendo hicho kitahitajia adhabu kama adhabu ya kufanya zinaa au inatosheleza kuomba msamaha?
Jibu: Tawbah na kuomba msamaha kunatosheleza. Vilevile ahifadhi swalah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alijiwa na mtu ambaye alikuwa amefanya kila kitu na mwanamke mmoja isipokuwa jimaa tu, mtu huyu akaja kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kumuuliza. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akakaa kimywa mpaka kulipoteremsha Kauli Yake (Ta´ala):
وَأَقِمِ الصَّلَاةَ طَرَفَيِ النَّهَارِ وَزُلَفًا مِّنَ اللَّيْلِ ۚ إِنَّ الْحَسَنَاتِ يُذْهِبْنَ السَّيِّئَاتِ ۚ ذَٰلِكَ ذِكْرَىٰ لِلذَّاكِرِينَ
“Simamisha swalah katika ncha mbili za mchana na sehemu ya kwanza ya usiku; hakika mema yanaondosha mabaya. Hivyo ni ukumbusho kwa wanaokumbuka.” (11:114)
Mtu yule akamuuliza: “Ee Mtume wa Allaah! Aayah hii inanihusu mimi mwenyewe au watu wote?” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akajibu na kusema:
“Ni kwa watu wote.”
Mwenye kuhifadhi swalah za faradhi Allaah kwa swalah hizo anamsamehe madhambi madogo madogo – himdi zote anastahiki Allaah.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Duruus-ul-Haram http://www.alfawzan.af.org.sa/node/13382
- Imechapishwa: 24/06/2020
Swali: Mtu ambaye shaytwaan amemshawishi na akamwende mwanamke ambaye ni ajinabi na mapenzi bila ya jimaa kitendo hicho kitahitajia adhabu kama adhabu ya kufanya zinaa au inatosheleza kuomba msamaha?
Jibu: Tawbah na kuomba msamaha kunatosheleza. Vilevile ahifadhi swalah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alijiwa na mtu ambaye alikuwa amefanya kila kitu na mwanamke mmoja isipokuwa jimaa tu, mtu huyu akaja kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kumuuliza. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akakaa kimywa mpaka kulipoteremsha Kauli Yake (Ta´ala):
وَأَقِمِ الصَّلَاةَ طَرَفَيِ النَّهَارِ وَزُلَفًا مِّنَ اللَّيْلِ ۚ إِنَّ الْحَسَنَاتِ يُذْهِبْنَ السَّيِّئَاتِ ۚ ذَٰلِكَ ذِكْرَىٰ لِلذَّاكِرِينَ
“Simamisha swalah katika ncha mbili za mchana na sehemu ya kwanza ya usiku; hakika mema yanaondosha mabaya. Hivyo ni ukumbusho kwa wanaokumbuka.” (11:114)
Mtu yule akamuuliza: “Ee Mtume wa Allaah! Aayah hii inanihusu mimi mwenyewe au watu wote?” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akajibu na kusema:
“Ni kwa watu wote.”
Mwenye kuhifadhi swalah za faradhi Allaah kwa swalah hizo anamsamehe madhambi madogo madogo – himdi zote anastahiki Allaah.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Duruus-ul-Haram http://www.alfawzan.af.org.sa/node/13382
Imechapishwa: 24/06/2020
https://firqatunnajia.com/kufanya-mapenzi-bila-ya-jimaa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)