Tumeulizwa ni ipi hukumu kwa mwenye kusema mimi ´Aqiydah yangu ni Salaf na Manhaj yangu ni fulani? ´Aqiydah yangu ni Salaf na Manhaj ya al-Ikhwaan?

Vipi utaifarikanisha Dini? Dini ni ´Aqiydah na Mahaj. Vipi utatenganisha kati ya hayo mawili? Isitoshe, Manhaj hii ambayo umechagua maana yake ni kwamba Salafiyyuun Manhaj yao imeharibika katika Da´wah, uelewa, dalili na al-Walaa´ wal-Baraa´? Lau ungelichukua Manhaj ya watu wa mwanzo, Manhaj ya Ahmad bin Hanbal, Ibn Taymiyyah na wengineo ungeliafikiana na ndugu zako ambao unawaita kuwa ni majasusi na vibaraka. Lau tutawaangalia kupitia Manhaj hii, porojo hizi za uongo zingelitoweka. Lakini tatizo ni kwamba wewe unawatazama Salafiyyuun kupitia Manhaj ya Khawaarij, siasa ya kimagharibi na mitazamo khabithi. Ndio maana umepata picha mbaya juu yao. Lakini hata hivyo, lau ungeliwatazama – Salafiyyuun wa kihakika – kupitia uongofu wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na yale waliyokuwemo Salaf, ungelipata kuona wao ndio wenye picha nzuri kabisa na kwamba wao ndio watu wa haki na wakati huo huo ukaona kuwa wewe ndio uko katika upotevu na upindaji, sawa katika ´Aqiydah au ´Aqiydah na Manhaj.

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://subulsalam.com/play.php?catsmktba=26874
  • Imechapishwa: 19/05/2015