Imaam al-Aajjuriy (aliyefariki 360 H) amesema:

“Khawaarij ndio [viumbe] walionajisika zaidi na wale walio katika madhehebu yao katika Khawaarij wengine… “

Anayesema “Mwenye kumtii kiongozi mwenye kutunga sheria kwenye kitu kimoja, ametoka katika Uislamu”. Yeye mwenyewe anajihukumu ukafiri kwa kuwa amewatii katika mambo mengi. Sio katika kitu kimoja tu, bali katika mambo mengi. Haya yamesemwa na Sayyid Qutwub. Ni mtu ambaye alikuwa ananyoa ndevu zake. Amemtii nani? Je, amemtii Allaah kwa kunyoa ndevu zake na kuvaa karvanti na mambo chungu mzima katika fikira na ´Aqiydah? Huyu masikini anajihukumu mwenyewe ukafiri pasina kujua. Haya ni madhehebu khatari sana, enyi ndugu.

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://subulsalam.com/play.php?catsmktba=26874
  • Imechapishwa: 19/05/2015