Jipime maarifa yako kuhusu twahara na swalah
Chemsha Bongo ya twahara na swalah 04
15:00
Kuna udhuru gani wa mwanaume kuacha kuswali mkusanyiko msikitini?
- Kazi muhimu za nyumbani
- Kufuatilia mambo ya kielimu
- Ugonjwa au khofu
Ni ipi hukumu ya kufanya manuizi kwa kutamka kwa sauti kavla ya swalah?
- Ni Sunnah
- Inapendeza
- Ni Bid'ah haijathibiti
Kuanza kwa Ramadhaan kunathibiti kwa ushahidi wa watu wangapi waadilifu?
- Mtu mmoja
- Watu watatu
- Watu watano
Ni lini mwisho wa wakati wa swalah ya Ishaa?
- Saa sita usiku
- Kunapokuwa giza kali
- Katikati ya usiku
Ni ipi hukumu ya ambaye amekumbuka swalah aliyokosa baada ya siku 2?
- Imeshapita na hatoiswali tena
- Atasamehewa kwa.s alisahau
- Ataiswali pale tu atapoikumbuka
Unachenguka wudhuu wa ambaye amekula nyamafu?
- Ndio kabisa
- Hapana
- Ndio, isipokuwa tu kama ni wa mnyama halali kumla
Kila ambaye inafaa kukusanya swalah anatakiwa vilevile kufupisha swalah?
- Ndio, kwa.s ni mambo yanayoenda sambamba
- Hapana, si lazima iwe hivo
- Inategemea na swalah
Swalah ya Dhuhr ina Sunnah (Rawaatib) ngapi kabla na baada yake?
- Kabla 2 na baada 4
- Kabla 2 na baada 3
- Kabla 2 au 4 na baada 2
Ni ipi katika hizi ni swalah ya kuomba kuteremshiwa mvua?
- Kusuuf
- Khusuuf
- Istisqaa'
Je, ipi hukumu ya kutaja jina la Allaah kabla ya kuanza kutawadha?
- Lazima na vinginevyo wudhuu' hausihi
- Ni Bid'ah potofu
- Ni wajibu, japo kuna wanaosema pia kuwa ni Sunnah
Ni ipi katika hizi ni swalah ya kuomuomba Allaah mwongozo (ushauri) wakati unaposhindwa kuamua moja katika mambo mawili?
- Istikhaarah
- Istisqaa'
- Khawf
Vipi kuswali kitambo kidogo kabla ya kuingia wakati wa swalah?
- Swalah haisihi na lazima airudi
- Swalah inasihi kama ni kitambo kidogo
- Swalah inasihi kama ni zile za kusoma kwa sauti na si zile za kusoma kimyakimya
Lini unaanza wakati wa kuswali Dhuhaa na ina Rakah ngapi?
- Baada ya Fajr na Rak'ah zake ni 4
- Baada ya Dhuhr na Rak'ah zake ni 2
- Baada ya takriban robo saa kuanzia kuchomoza kwa jua na Rak'ah zake ni 8
Ni kipi katika haya ni mojawapo ya nguzo za swalah?
- Kusoma kwa utaratibu (tartiyl) ipasavyo
- Kutulizana kwenye nguzo zote
- Kufanya heshima na swalah
Ni sahihi msemo unaosema kwamba Sutrah ya imamu ni Sutrah ya maamuma?
- Hapana
- Inategemea na nia ya imamu
- Ndio
Nani anayetangulizwa mbele kuwa imamu kati ya aliyehifadhi mvuta sigara na anavaa isbaal na mwingine amehifadhi kiasi lakini anafuata Sunnah?
- Imamu mwenye isbaal
- Imamu anayefuata Sunnah
- Yeyote tu ni sawa
Swalah ni nguzo ya ngapi katika zile nguzo tano za Uislamu?
- Ya 3
- Ya 2
- Ya 5
Ni ipi hukumu ya kuswali nyuma ya imamu unayemjua anapiga rimli (mganga)?
- Haina neno dhambi ni zake
- Haifai kabisa
- Inategemea na nia yako
Lini unamalizika muda wa Dhuhaa?
- Kabla ya takriban robo saa jua kupondoka
- Mpaka ikiingia 'Aswr
- Masaa mawili kuanzia kuchomoza kwa jua
Ni lini inaswaliwa Sunnah (Raatibah) ya kabla ya Fajr?
- Kabla ya Fajr kwa dakika 10
- Baada ya kuingia muda wa Fajr
- Saa 06.00 asubuhi
Je, swalah inasihi nyuma ya imamu mnyoa ndevu?
- Ndio
- Hapana kwa.s kunyoa ndevu ni dhambi kubwa
- Inasihi kama imamu hana madhambi mengine makubwa
Ni lini mtoto huanza kuamrishwa kuswali?
- Anapokuwa na miaka 7
- Anapokuwa na miaka 5
- Anapokuwa na miaka 12