Swali: Mwanamke anatumia dawa ya kichwa na ndani yake kuna asilimia kidogo ya poimbe. Je, inajuzu?
Jibu: Ikiwa ndani kuna kilevi haifai kuitumia kama dawa:
“Kingi kinacholevya basi kidogo chake pia ni haramu.”
Swali: Vipi ikiwa dawa hiyo inatumiwa nje ya mwili na hailiwi wala kunywewa?
Jibu: Haijalishi kitu. Udhahiri wa Sunnah ni kwamba inakatazwa. Kwa sababu kupatikana kwake ni njia inayopelekea kunywewa na kuliwa.
Swali: Vipi yale yanayonasibishwa kwa Shaykh-ul-Islaam (Rahimahu Allaah) kwamba amejuzisha hilo?
Jibu: Sidhihirikiwi na kitu. Kinacholevya hakitumiwi. Ambacho kina kileo hakitumiwi. Ni mamoja kinatumiwa kama mafuta, kichwani wala dawa:
“Enyi waja wa Allaah, jitibisheni! Na wala msijitibishe kwa haramu.”
Swali: Hukumu ni hiyohiyo juu ya manukato yaliyo na asilimia kidogo ya pombe? an
Jibu: Ndio. Tumefikiwa na khabari kwamba manukato yanayoitwa ´cologne` ndani yake kuna pombe na kileo.
Swali: Baadhi yake ni asilimia ndogo?
Jibu: Kukipatikana ndani yake kileo yaepukwe. Yasitumiwe ikitambulika kuwa ndani kuna kileo kinachotumiwa na watu.
Swali: Maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kila kinacholevya ni haramu.”
Vipi kukitumia kwa njia ya kujitibisha?
Jibu: Kila kileo ni pombe na kila kileo ni haramu. Kingi kinacholevya basi kidogo chake pia ni haramu.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23624/حكم-الكحول-في-الطيب-والدواء
- Imechapishwa: 05/03/2024
Swali: Mwanamke anatumia dawa ya kichwa na ndani yake kuna asilimia kidogo ya poimbe. Je, inajuzu?
Jibu: Ikiwa ndani kuna kilevi haifai kuitumia kama dawa:
“Kingi kinacholevya basi kidogo chake pia ni haramu.”
Swali: Vipi ikiwa dawa hiyo inatumiwa nje ya mwili na hailiwi wala kunywewa?
Jibu: Haijalishi kitu. Udhahiri wa Sunnah ni kwamba inakatazwa. Kwa sababu kupatikana kwake ni njia inayopelekea kunywewa na kuliwa.
Swali: Vipi yale yanayonasibishwa kwa Shaykh-ul-Islaam (Rahimahu Allaah) kwamba amejuzisha hilo?
Jibu: Sidhihirikiwi na kitu. Kinacholevya hakitumiwi. Ambacho kina kileo hakitumiwi. Ni mamoja kinatumiwa kama mafuta, kichwani wala dawa:
“Enyi waja wa Allaah, jitibisheni! Na wala msijitibishe kwa haramu.”
Swali: Hukumu ni hiyohiyo juu ya manukato yaliyo na asilimia kidogo ya pombe? an
Jibu: Ndio. Tumefikiwa na khabari kwamba manukato yanayoitwa ´cologne` ndani yake kuna pombe na kileo.
Swali: Baadhi yake ni asilimia ndogo?
Jibu: Kukipatikana ndani yake kileo yaepukwe. Yasitumiwe ikitambulika kuwa ndani kuna kileo kinachotumiwa na watu.
Swali: Maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kila kinacholevya ni haramu.”
Vipi kukitumia kwa njia ya kujitibisha?
Jibu: Kila kileo ni pombe na kila kileo ni haramu. Kingi kinacholevya basi kidogo chake pia ni haramu.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23624/حكم-الكحول-في-الطيب-والدواء
Imechapishwa: 05/03/2024
https://firqatunnajia.com/pombe-kwenye-dawa-na-manukato/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)