Swali: Mwandishi wa “Manhaj-ul-Anbiyaa´ fiyd-Da´wah ilaa Allaah” amesema:
“Nimesoma vitabu vya ´Aqiydah na kuona kuwa vyote si vyenye kuridhisha. Kwa sababu vina Hadiyth tu, maandiko na hukumu.”
Unasemaje juu ya hilo?
Jibu: Hili ni kosa kubwa. Vyote haviridhishi? Namuomba kinga Allaah. Vitabu vya ´Aqiydah sahihi sio vyenye kuchosha. Humo mnanukuliwa aliyosema Allaah na Mtume Wake. Ikiwa anamaanisha kuwa Qur-aan na Sunnah ni vyenye kuchosha huku ni kuritadi kutoka katika Uislamu. Maneno haya ni ya kigonjwa na machafu.”
Swali: Ni ipi hukumu ya kuuza kitabu hiki?
Jibu: Ikiwa mna maneno haya haijuzu kukiuza. Ni wajibu kukipasua ikiwa maneno hayo yamo humo.”
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Muhadhara “Aafaat-ul-Lisaan”, 1413-12-29, uliofanywa Twaaif
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)