Jengine ni kwamba napenda kuzindua kitu kinachotumiwa na watu wengi pasi na wao kujua kuwa ndani yake mna kileo. Mfano wa bia. Hata kama wanasema kuwa haina kileo hawatakiwi kusadikishwa. Mfano mwingine ni matibabu yenye kileo. Nimepewa khabari kuwa dawa nyingi za kunywa zina kileo. Vivyo hivyo manukato yenye kileo, kwa sababu mwenye kujitia manukato amebaba na kununua pombe. Imekwishatangulia kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah ameilaani pombe na mwenye kuinywa, mwenye kuihudumia, mwenye kuiuza, mwenye kuinunua, mwenye kuitengeneza, mwenye kutengenezewa, mwenye kuoda na kula thamani yake.”[1]
Ikiwa pombe ni haramu basi ni haramu vilevile kuiuza.
[1] Abu Daawuud na al-Haakim. Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh-ul-Jaamiy´” (5091).
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 274
- Imechapishwa: 15/04/2025
Jengine ni kwamba napenda kuzindua kitu kinachotumiwa na watu wengi pasi na wao kujua kuwa ndani yake mna kileo. Mfano wa bia. Hata kama wanasema kuwa haina kileo hawatakiwi kusadikishwa. Mfano mwingine ni matibabu yenye kileo. Nimepewa khabari kuwa dawa nyingi za kunywa zina kileo. Vivyo hivyo manukato yenye kileo, kwa sababu mwenye kujitia manukato amebaba na kununua pombe. Imekwishatangulia kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah ameilaani pombe na mwenye kuinywa, mwenye kuihudumia, mwenye kuiuza, mwenye kuinunua, mwenye kuitengeneza, mwenye kutengenezewa, mwenye kuoda na kula thamani yake.”[1]
Ikiwa pombe ni haramu basi ni haramu vilevile kuiuza.
[1] Abu Daawuud na al-Haakim. Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh-ul-Jaamiy´” (5091).
Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 274
Imechapishwa: 15/04/2025
https://firqatunnajia.com/pombe-dawa-za-kunywa-na-manukato-yasiyo-na-kileo/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)