Swali: Kuvaa pete ni Sunnah au inaruhusu tu?
Jibu: Maoni ya karibu zaidi – na Allaah ndiye mjuzi zaidi – ni kwamba ni Sunnah kwa watawala. Kuhusu watu wa kawaida tunafupizika kusema kwamba inaruhusu. Hata hivyo kwa watawala ni Sunnah. Mosi kwa ajili ya kumuiga Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), pili ili waweze kupiga kwayo muhuri kwenye nyaraka mbalimbali. Imepokelewa kwenye upokezi wa Abu Daawuud kupitia kwa Abu Rihaanah makatazo ya kuvaa pete isipokuwa tu kwa watawala. Hata hivyo kuna kasoro katika kusihi kwake. Lakini inafasiriwa namna hii endapo imesihi.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24433/حكم-اتخاذ-الخاتم
- Imechapishwa: 25/10/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket