Swali: Nini maana ya maneno ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumwambia ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anh):
“Usiache picha isipokuwa umeiharibu na wala kaburi lililonyanyuliwa isipokuwa umelisawazisha.”[1]?
Leo tunaona makaburi mengi yameinuliwa zaidi ya shibri moja.
Jibu: Kaburi lililoinuliwa ni lile linalokuwa juu tofauti kuliko makaburi mengine. Kaburi kama hili ni wajibu kusawazishwa na mengine ili watu wasije kufitinishwa nalo. Watu wakiona kaburi hili liko juu kuliko mengine yote kuna khatari wakafitinishwa nalo. Kwa ajili hii ndio maana Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimtuma ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anh) ayasawazishe makaburi yote yaliyoinuliwa.
[1] Muslim (969).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/186)
- Imechapishwa: 26/08/2021
Swali: Nini maana ya maneno ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumwambia ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anh):
“Usiache picha isipokuwa umeiharibu na wala kaburi lililonyanyuliwa isipokuwa umelisawazisha.”[1]?
Leo tunaona makaburi mengi yameinuliwa zaidi ya shibri moja.
Jibu: Kaburi lililoinuliwa ni lile linalokuwa juu tofauti kuliko makaburi mengine. Kaburi kama hili ni wajibu kusawazishwa na mengine ili watu wasije kufitinishwa nalo. Watu wakiona kaburi hili liko juu kuliko mengine yote kuna khatari wakafitinishwa nalo. Kwa ajili hii ndio maana Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimtuma ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anh) ayasawazishe makaburi yote yaliyoinuliwa.
[1] Muslim (969).
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/186)
Imechapishwa: 26/08/2021
https://firqatunnajia.com/nini-maana-ya-kaburi-lililoinuliwa-kunyanyuliwa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)