Swali: Ni ipi hukumu ya mwenye kusema “Hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah! Uso wa Allaah ndio wenye kudumu!” wakati wa kuliandama jeneza kwa sauti ya juu na wakati wa kuzika wanasema “Ee Mwingi wa Rahmah! Ee Mwingi wa Rahmah!”? Ni ipi Sunnah wakati wa kusindikiza jeneza na wakati wa kumzika maiti?
Jibu: Ni Bid´ah. Hapana shaka ya kwamba hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah na kwamba hakuna atayebaki isipokuwa Yeye pekee. Hata hivyo ni Bid´ah kusema yale yote yaliyotajwa kwenye swali. Kila ´ibaadah ambayo haikufanywa na Salaf ni Bid´ah. Vilevile ni Bid´ah kusema “Ee Mwingi wa Rahmah! Ee Mwingi wa Rahmah!” wakati wa kuzika.
Sunnah wakati wa kulisindikiza jeneza ni mtu kuzingatia na kufikiria mwisho wake. Hivi sasa anaenda kwenye jeneza, kesho jeneza hili litambeba yeye. Ayazingatie matendo yake na hali yake.
Kuhusu wakati wa kuzika, Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipokuwa akimaliza kuzika alikuwa akisema:
“Muombeeni msamaha ndugu yenu na mumtakie uthabiti, hakika hivi sasa ataulizwa.”[1]
Haya ndio yamewekwa katika Shari´ah.
[1] Abu Daawuud (3221).
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/165)
- Imechapishwa: 24/08/2021
Swali: Ni ipi hukumu ya mwenye kusema “Hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah! Uso wa Allaah ndio wenye kudumu!” wakati wa kuliandama jeneza kwa sauti ya juu na wakati wa kuzika wanasema “Ee Mwingi wa Rahmah! Ee Mwingi wa Rahmah!”? Ni ipi Sunnah wakati wa kusindikiza jeneza na wakati wa kumzika maiti?
Jibu: Ni Bid´ah. Hapana shaka ya kwamba hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah na kwamba hakuna atayebaki isipokuwa Yeye pekee. Hata hivyo ni Bid´ah kusema yale yote yaliyotajwa kwenye swali. Kila ´ibaadah ambayo haikufanywa na Salaf ni Bid´ah. Vilevile ni Bid´ah kusema “Ee Mwingi wa Rahmah! Ee Mwingi wa Rahmah!” wakati wa kuzika.
Sunnah wakati wa kulisindikiza jeneza ni mtu kuzingatia na kufikiria mwisho wake. Hivi sasa anaenda kwenye jeneza, kesho jeneza hili litambeba yeye. Ayazingatie matendo yake na hali yake.
Kuhusu wakati wa kuzika, Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipokuwa akimaliza kuzika alikuwa akisema:
“Muombeeni msamaha ndugu yenu na mumtakie uthabiti, hakika hivi sasa ataulizwa.”[1]
Haya ndio yamewekwa katika Shari´ah.
[1] Abu Daawuud (3221).
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/165)
Imechapishwa: 24/08/2021
https://firqatunnajia.com/ni-ipi-sunnah-wakati-wa-kulisindikiza-jeneza-na-wakati-wa-kuzika/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)