Swali: Ni ipi hukumu ya kuyaomba msaada makaburi ya mawalii, kutufu kwayo, kutafuta baraka kwa miti yake, kuyawekea nadhiri, kujidhalilisha kwenye makaburi yao na kumuomba Allaah kupitia kwayo?
Jibu: Kuyaomba msaada makaburi ya mawalii, kuyawekea nadhiri, kumuomba Allaah kupitia kwa maiti hao ni shirki kubwa. Shirki hiyo inamtoa mwenye nayo katika Uislamu. Shirki hiyo inawajibisha kumuweka milele Motoni yule mwenye kufa juu yake.
Kuhusu kutufu kwenye makaburi au kujidhalilisha kwayo ni Bid´ah. Ni haramu kufanya hivo. Ni njia kubwa inayopelekea kumuabudu mwenye kaburi hilo badala ya Allaah. Vilevile inaweza kuwa shirki kwa dhati yake ikiwa kama kwa kufanya hivo ataamini kuwa maiti analeta manufaa au kumzuia na madhara au kutufu kwake akakusudia kujikurubisha kwa maiti huyo.
- Mhusika: al-Najnah ad-Daaimah
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa al-Najnah ad-Daaimah (01/113-114)
- Imechapishwa: 06/10/2020
Swali: Ni ipi hukumu ya kuyaomba msaada makaburi ya mawalii, kutufu kwayo, kutafuta baraka kwa miti yake, kuyawekea nadhiri, kujidhalilisha kwenye makaburi yao na kumuomba Allaah kupitia kwayo?
Jibu: Kuyaomba msaada makaburi ya mawalii, kuyawekea nadhiri, kumuomba Allaah kupitia kwa maiti hao ni shirki kubwa. Shirki hiyo inamtoa mwenye nayo katika Uislamu. Shirki hiyo inawajibisha kumuweka milele Motoni yule mwenye kufa juu yake.
Kuhusu kutufu kwenye makaburi au kujidhalilisha kwayo ni Bid´ah. Ni haramu kufanya hivo. Ni njia kubwa inayopelekea kumuabudu mwenye kaburi hilo badala ya Allaah. Vilevile inaweza kuwa shirki kwa dhati yake ikiwa kama kwa kufanya hivo ataamini kuwa maiti analeta manufaa au kumzuia na madhara au kutufu kwake akakusudia kujikurubisha kwa maiti huyo.
Mhusika: al-Najnah ad-Daaimah
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa al-Najnah ad-Daaimah (01/113-114)
Imechapishwa: 06/10/2020
https://firqatunnajia.com/ni-ipi-hukumu-ya-kuyaomba-na-kutufu-kwenye-makaburi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)