Ni ipi hukumu ya kutangamana na mtu anayechezea dini shere?

Swali: Ni ipi hukumu ya kutangamana na mtu anayechezea dini shere?

Jibu: Anayeifanyia istihzai dini anaritadi kutoka nje katika Uislamu. Haijalishi kitu japokuwa atadai kuwa anafanya hivo kwa sababu ya mzaha tu. Haijuzu kufanya utani kwa mambo kama haya. Amesema (Ta´ala):

وَلَئِن سَأَلْتَهُمْ لَيَقُولُنَّ إِنَّمَا كُنَّا نَخُوضُ وَنَلْعَبُ ۚ قُلْ أَبِاللَّـهِ وَآيَاتِهِ وَرَسُولِهِ كُنتُمْ تَسْتَهْزِئُونَ لَا تَعْتَذِرُوا قَدْ كَفَرْتُم بَعْدَ إِيمَانِكُمْ

“Ukiwauliza watasema: “Hakika tulikuwa tunaporoja na tunacheza.” Sema: “Je, mlikuwa mnamfanyia istihizai Allaah na Aayah Zake na Mtume Wake?” Hivyo basi msitoe udhuru. Kwani mmekwishakufuru baada ya kuamini kwenu.” (09:65.66)

Mwenye kufanya mzaha na dini hapana shaka kwamba ameritadi kutoka katika Uislamu. Hata kama atakuwa mwenye kufanya mzaha. Hapa sio sehemu ya kucheza shere.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Thalaath-il-Usuwl (05) http://ajurry.com/safrawy/chorohat-elakida/charh-el-osol-el-thalatha/charh-fwzan/05.mp3
  • Imechapishwa: 18/01/2019