Swali: Ni ipi hukumu ya kutaja mazuri ya maiti? Ni ipi hukumu ya kumuombea du´aa baada ya kuzikwa? Ni ipi hukumu ya kuwaomba wahudhuriaji wamuombee?
Jibu: Kutaja mazuri ya maiti hakuna neno midhali sio kwa njia ya kuomboleza. al-Haakim amepokea katika “al-Mustadrak” yake kupitia kwa Jaabir (Radhiya Allaahu ´anh) aliyesema:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa katika mazishi ya Banuu Salamah na mimi nilikuwa karibu naye. Baadhi yao wakasema: “Ee Mtume wa Allaah! Alikuwa mwanaume mzuri. Alikuwa ni muislamu safi.” Wakamsifu vizuri ambapo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Wewe unasemaje?” Mtu yule akasema: “Allaah ndiye anajua yale yaliyofichikana.”[1]
Kuhusu kumuombea maiti baada ya mazishi au kuomba du´aa, Abu Daawuud amepokea ya kwamba ´Uthmaan bin ´Affaan (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipokuwa anapomaliza kumzika maiti husimama na kusema: “Muombeeni msamaha ndugu yenu na mumtakie uthabiti. Hakika hivi sasa ataulizwa.”[2]
Mtu akifanya hivo na mfano wake haina neno.
[1] Tazama ”Tafsiyr al-Qur-aan al-´Adhwiym” (1/348) ya Ibn Kathiyr.
[2] Abu Daawuud (3221).
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/236)
- Imechapishwa: 02/09/2021
Swali: Ni ipi hukumu ya kutaja mazuri ya maiti? Ni ipi hukumu ya kumuombea du´aa baada ya kuzikwa? Ni ipi hukumu ya kuwaomba wahudhuriaji wamuombee?
Jibu: Kutaja mazuri ya maiti hakuna neno midhali sio kwa njia ya kuomboleza. al-Haakim amepokea katika “al-Mustadrak” yake kupitia kwa Jaabir (Radhiya Allaahu ´anh) aliyesema:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa katika mazishi ya Banuu Salamah na mimi nilikuwa karibu naye. Baadhi yao wakasema: “Ee Mtume wa Allaah! Alikuwa mwanaume mzuri. Alikuwa ni muislamu safi.” Wakamsifu vizuri ambapo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Wewe unasemaje?” Mtu yule akasema: “Allaah ndiye anajua yale yaliyofichikana.”[1]
Kuhusu kumuombea maiti baada ya mazishi au kuomba du´aa, Abu Daawuud amepokea ya kwamba ´Uthmaan bin ´Affaan (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipokuwa anapomaliza kumzika maiti husimama na kusema: “Muombeeni msamaha ndugu yenu na mumtakie uthabiti. Hakika hivi sasa ataulizwa.”[2]
Mtu akifanya hivo na mfano wake haina neno.
[1] Tazama ”Tafsiyr al-Qur-aan al-´Adhwiym” (1/348) ya Ibn Kathiyr.
[2] Abu Daawuud (3221).
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/236)
Imechapishwa: 02/09/2021
https://firqatunnajia.com/ni-ipi-hukumu-ya-kutaja-mazuri-ya-maiti/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)