Swali: Ni ipi hukumu ya kusindikiza jeneza la muislamu? Ni wajibu kwa waislamu wote?
Jibu: Wanachuoni wanasema kumuosha maiti, kumvisha sanda, kumbeba na kumzika ni wajibu kwa baadhi ya waislamu. Kukipatikana wataofanya hayo hakuna haja ya wengine kufanya hivo. Lakini Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekokoteza kushiriki katika kulisindikiza jeneza na kusema:
“Atayelishuhudia jeneza mpaka likaswaliwa, basi ana Qiraatw. Na yule atayelishuhudia mpaka likazikwa, ana Qiraatw mbili.” Kukasemwa: “Qiraatw mbili ni nini?” Akasema: “Ni mfano wa milima miwili mikubwa.”[1]
[1] al-Bukhaariy (1325) na Muslim (945).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/167-168)
- Imechapishwa: 25/08/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket