Swali: Ni ipi hukumu ya kufungua mafundo na kufunua uso wa maiti pindi anapowekwa ndani ya kaburi?
Jibu: Kuhusu kufungua mafundo, imepokelewa ya kwamba ´Abdullaah bin Mas´uud (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Mnapomuweka maiti ndani ya kaburi fungueni mafundo.”[1]
Kuhusu inapokuja katika kufunua uso wote wa maiti, ni jambo lisilo na asli. Kubwa lililopokelewa – kama itakuwa ni Swahiyh – ni maneno ya ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh):
“Nitapofariki na mkaniweka ndani ya kaburi, liacheni shavu langu liguse ardhi.”[2]
[1] Mtunzi wa “ar-Rawdhw al-Murbi´” amemnasibishia upokezi huu al-Athram na akasema kwenye taaliki: “Mfano wa haya yamepokelewa kutoka kwa Samurah.”
[2] Tazama ”al-Mughniy” (3/428) ya Ibn Qudaamah.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/183)
- Imechapishwa: 25/08/2021
Swali: Ni ipi hukumu ya kufungua mafundo na kufunua uso wa maiti pindi anapowekwa ndani ya kaburi?
Jibu: Kuhusu kufungua mafundo, imepokelewa ya kwamba ´Abdullaah bin Mas´uud (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Mnapomuweka maiti ndani ya kaburi fungueni mafundo.”[1]
Kuhusu inapokuja katika kufunua uso wote wa maiti, ni jambo lisilo na asli. Kubwa lililopokelewa – kama itakuwa ni Swahiyh – ni maneno ya ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh):
“Nitapofariki na mkaniweka ndani ya kaburi, liacheni shavu langu liguse ardhi.”[2]
[1] Mtunzi wa “ar-Rawdhw al-Murbi´” amemnasibishia upokezi huu al-Athram na akasema kwenye taaliki: “Mfano wa haya yamepokelewa kutoka kwa Samurah.”
[2] Tazama ”al-Mughniy” (3/428) ya Ibn Qudaamah.
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/183)
Imechapishwa: 25/08/2021
https://firqatunnajia.com/ni-ipi-hukumu-ya-kufungua-mafundo-na-kufunua-uso-wa-maiti-ndani-ya-kaburi/