Swali: Ni bora kuswali Sunnah ya ijumaa nyumbani au msikitini?
Jibu: Swalah zinazopendeza zote bora ni kuziswali nyumbani. Lakini hapana vibaya akiziswali msikitini. Zote ni bora kuziswali nyumbani. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Swalah bora ya mtu ni nyumbani kwake isipokuwa ya faradhi.”
Swali: Kuna tofauti gani inapokuja katika Sunnah ya ijumaa mtu kuiswali msikitini Rak´ah nne na nyumbani Rak´ah mbili? Je, utofautishaji unasihi?
Jibu: Msingi ni yale aliyoeleza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Mwenye kutaka kuswali baada ya ijumaa basi aswali baada yake [Rak´ah] nne.”
Sunnah ni Rak´ah nne. Kamilifu zaidi ni mtu kuswali Rak´ah nne; ni mamoja nyumbani au msikitini. Imekuja katika tamko jingine:
“Mkiswali baada ya ijumaa basi mswali baada yake [Rak´ah] nne.”
Ameipokea Muslim.
Swali: Amri hii inafahamisha kuwa ni lazima?
Jibu: Hapana. Ni kwa yule anayetaka kuswali.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22571/هل-الافضل-لسنة-الجمعة-البيت-ام-المسجد
- Imechapishwa: 04/07/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)