Naaswir al-´Umar ni katika Khawaarij wakaaji

Swali: Kuna kitabu cha mapinduzi kinachoitwa “at-Tarbiyah al-Jihaadiyyah” na kimepigwa marufuku na nchi kutokana na khatari yake. Naaswir al-´Umar amependekeza kitabu hichi na kurejea kwacho pamoja na kwamba kitabu hichi kina maelekezo ya Khawaarij na kuanzisha vita dhidi ya mamlaka. Unasemaje juu ya hilo?

Jibu: Kwa kifupi Naaswir al-´Umar ni katika wao ikiwa kama ni kweli. Anajulikana kujishughulisha kwake na mambo ya kisasa.

´Aa´idh al-Qarniy amemsifu na kusema kwama hakuna yeyote ambaye amebobea katika mambo ya kisasa kama Shaykh Naaswir al-´Umar. Anamlinganisha na ash-Shaafi´iy. ash-Shaafi´iy alikuwa wa kwanza ambaye alibobea katika Usuul-ul-Fiqh wakati Naaswir al-´Umar kwa mujibu wake ndio wa kwanza ambaye amebobea katika mambo ya kisasa. Wanachuoni wamemjeruhi na makosa yake. Amesimama kwa ufupi kwa kuwa wanachuoni hawafahamu mambo ya kisasa. Sio jambo la ajabu kwa kupendekeza kitabu hichi kilichotajwa kwa kuwa mwandishi ameafikiana na matamanio yake. Pamoja na yote hayo ni mmoja katika viongozi wa mapinduzi na vurugu za kisasa na katika Khawaarij wakaazi.

  • Mhusika: Shaykh ´Ubayd bin ´Abdillaah al-Jaabiriy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=128881
  • Imechapishwa: 23/07/2020