Swali: Tangu utotoni mwangu nilikuwa naishi na chembe ya moyo na kuvuja damu kwa ndani:
1 – Je, nina thawabu juu ya hilo kwa sababu nimekosa ujana wangu na afya yangu?
2 – Mara nyingi huswali kwa Tayammum kwa sababu siwezi kuoga. Je, inafaa kwangu kufanya hivo?
3 – Je, naweza kuwafunza wanafunzi Qur-aan pasi na twahara?
Jibu:
1 – Ukifanya subira kwa yale yaliyokupata basi unapata thawabu mbele ya Allaah. Ukikata tamaa na usisubiri basi unanyimwa thawabu.
2 – Ukweli wa mambo ikiwa ni vile ulivosema kwamba huwezi kuoga, basi imesuniwa kwako kufanya Tayammum kutokana na janaba.
3 – Ikiwa huwezi kutumia maji katika twahara kutokana na hadathi, basi itakutosha kufanya Tayammum kwa ajili ya twahara kwa ajili ya kugusa msahafu. Baada ya hapo itafaa kwako kufunza Qur-aan ijapo utakuwa huna twahara kutokana na hadathi ndogo.
Kuhusu mwenye janaba haifai kwake kugusa msahafu, asisome Qur-aan na wala asiwafunze wanafunzi mpaka kwanza atwahirike.
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
´Abdur-Razzaaq ´Afiyfiy
´Abdullaah bin Ghudayyaan
´Abdullaah bin Qu´uud
- Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (05/380) nr. (8592)
- Imechapishwa: 05/06/2022
Swali: Tangu utotoni mwangu nilikuwa naishi na chembe ya moyo na kuvuja damu kwa ndani:
1 – Je, nina thawabu juu ya hilo kwa sababu nimekosa ujana wangu na afya yangu?
2 – Mara nyingi huswali kwa Tayammum kwa sababu siwezi kuoga. Je, inafaa kwangu kufanya hivo?
3 – Je, naweza kuwafunza wanafunzi Qur-aan pasi na twahara?
Jibu:
1 – Ukifanya subira kwa yale yaliyokupata basi unapata thawabu mbele ya Allaah. Ukikata tamaa na usisubiri basi unanyimwa thawabu.
2 – Ukweli wa mambo ikiwa ni vile ulivosema kwamba huwezi kuoga, basi imesuniwa kwako kufanya Tayammum kutokana na janaba.
3 – Ikiwa huwezi kutumia maji katika twahara kutokana na hadathi, basi itakutosha kufanya Tayammum kwa ajili ya twahara kwa ajili ya kugusa msahafu. Baada ya hapo itafaa kwako kufunza Qur-aan ijapo utakuwa huna twahara kutokana na hadathi ndogo.
Kuhusu mwenye janaba haifai kwake kugusa msahafu, asisome Qur-aan na wala asiwafunze wanafunzi mpaka kwanza atwahirike.
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
´Abdur-Razzaaq ´Afiyfiy
´Abdullaah bin Ghudayyaan
´Abdullaah bin Qu´uud
Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (05/380) nr. (8592)
Imechapishwa: 05/06/2022
https://firqatunnajia.com/mwenye-maradhi-ya-chembe-ya-moyo-na-kuvuja-damu-kwa-ndani-na-twahara/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)