Mwanamke mzee sana kusafiri bila Mahram

Swali: Je, inajuzu kwa mwanamke mzee sana kusafiri peke yake akiwa pamoja na kundi pamoja na kujua ya kwamba ana mume na Mahaarim?

Jibu: Ni mamoja mwanamke mzee, mdogo na aliye kati na kati:

“Si halali kwa mwanamke anayemwamini Allaah na siku ya Mwisho kusafiri isipokuwa awe pamoja naye Mahram.”

Hili linamgusa mwanamke sawa awe ni mzee au mdogo. Kutokana na ujumla ya kauli yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

“Si halali kwa mwanamke… “

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (54) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1431-11-03.mp3
  • Imechapishwa: 21/08/2020