Swali: Je, inafaa kwa mwanamke kufunga bila idhini ya mume wake mwezi usiokuwa Ramadhaan?
Jibu: Haijuzu kwa mwanamke kufunga pasi na idhini ya mumewe. Hilo ni kutokana na yale aliyopokea Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwanamke asifunge na mume wake yuko [hakusafiri] isipokuwa kwa idhini yake.”[1]
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) pia ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwanamke asifunge siku na mume wake yuko [hakusafiri] mbali na mwezi wa Ramadhaan isipokuwa kwa idhini yake.”[2]
Kutokana na hayo haifai kwa mwanamke kufunga swawm iliyopendekezwa isipokuwa kwa idhini yake. Kwa sababu swawm iliyopendekezwa ni Sunnah na haki ya mume ni wajibu. Kufunga kutamzuilia kutokamana na baadhi ya haki zake za wajibu juu yake mke.
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
´Abdul-´Aziyz Aalus-Shaykh
Swaalih al-Fawzaan
Bakr Abu Zayd
[1] al-Bukhaariy katika ”as-Swahiyh” yake. Tazama ”Fath-ul-Baariy” (09/293).
[2] Abu Daawuud katika ”as-Sunan” yake. Tazama ”´Awn-ul-Ma´abuud” (07/128) na Ibn Maajah katika “as-Sunan” yake (01/56).
- Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (19307)
- Imechapishwa: 08/05/2022
Swali: Je, inafaa kwa mwanamke kufunga bila idhini ya mume wake mwezi usiokuwa Ramadhaan?
Jibu: Haijuzu kwa mwanamke kufunga pasi na idhini ya mumewe. Hilo ni kutokana na yale aliyopokea Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwanamke asifunge na mume wake yuko [hakusafiri] isipokuwa kwa idhini yake.”[1]
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) pia ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwanamke asifunge siku na mume wake yuko [hakusafiri] mbali na mwezi wa Ramadhaan isipokuwa kwa idhini yake.”[2]
Kutokana na hayo haifai kwa mwanamke kufunga swawm iliyopendekezwa isipokuwa kwa idhini yake. Kwa sababu swawm iliyopendekezwa ni Sunnah na haki ya mume ni wajibu. Kufunga kutamzuilia kutokamana na baadhi ya haki zake za wajibu juu yake mke.
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
´Abdul-´Aziyz Aalus-Shaykh
Swaalih al-Fawzaan
Bakr Abu Zayd
[1] al-Bukhaariy katika ”as-Swahiyh” yake. Tazama ”Fath-ul-Baariy” (09/293).
[2] Abu Daawuud katika ”as-Sunan” yake. Tazama ”´Awn-ul-Ma´abuud” (07/128) na Ibn Maajah katika “as-Sunan” yake (01/56).
Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (19307)
Imechapishwa: 08/05/2022
https://firqatunnajia.com/mwanamke-kufunga-sunnah-bila-idhini-ya-mume-wake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)