Swali: Msichana wangu amekataa posa ya mposaji. Hoja yake eti anataka kukamilisha masomo yake ya chuo kikuu. Hivyo amekataa kuolewa kabisa. Je, nimuozeshe licha kukataa kwake au nimsubiri amalize masomo yake?
Jibu. Msubirie. Lakini hakikisha unamchunga na unamlinda kutokana na shari. Kwa sababu leo fitina ni nyingi. Hakikisha unamchunga na kumlinda mpaka akamilishe masomo yake. Lakini bora kwake ni yeye kuolewa. Kuolewa hakupingani na kusoma. Anaweza kumuwekea sharti mume wake amwache asome. Tatizo litakuwa limeondoka. Amwekee sharti akamilishe masomo yake. Hapo tatizo litakuwa limeondoka.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (36)
- Imechapishwa: 16/08/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)